Thursday, November 5, 2015

KUAPISHWA KWA RAIS DR.JOHN MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungao wa Tanzania Mh, Dk. John Pombe Magufuli akiwashukuru watanzania wote kwa kumchagua kuwa rais wa awamu ya tano, pia kawataka viongozi wa upinzani kushirikiana na serikali yake.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh, Dk. John Pombe Magufuri akisalimiana na Rais wa Zanzibar Dokta Ali Mohammed Shein katika Jukwaa la uwanja wa Taifa (Uhuru).

Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. JOHN POMBE MAGUFULI akila kiapo katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, ''Mimi John Pombe Magufuli naapa nitatenda kazi zangu za urais kwa mujibu wa sheria na mila na desturi za Jamhuri ya muungano wa Tanzania, ewe mwenyezi mungu nisaidie Amen.''  



Makamu wa rais wa Kwanza mwanamke nchini Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akiweka sahii ya kiapo katika Uwanja wa Taifa Jijin Dar es Salaam.


Posted By Emman